• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

“Bendera ya Ushindi Ipo Mikononi mwa Walimu” – Dkt. Mutahabwa

Imewekwa : May 2nd, 2024

“Bendera ya Ushindi Ipo Mikononi mwa Walimu” – Dkt. Mutahabwa

Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ni miongoni mwa Halmashauri zilizochaguliwa katika kuwajengea uwezo walimuu wa masomo ya Sayansi na Hisabati, ambapo kwa Halmashauri hiyo shule Tisa zimeweza kuchaguliwa na kushiriki mafunzo hayo.

Mafunzo hayo yalitolewa na Wahadhiri kutoka Chuo Kikuu Huria Tanzania ambayo yalifanyika Januari 30, 2024 katika Ukumbi wa Chuo Kikuu Huria Tawi la Iringa, ambapo yaliongozwa na Kamishina wa Elimu Tanzania Dkt. Lyabwene Mutahabwa na kutoa Kauli Mbiu hiyo ya “Bendera ya Ushindi Ipo Mikononi mwa Walimu”.

Lengo la Mafunzo hayo ilikuwa ni kuwajengea Walimu uwezo na ubunifu na mafunzo ya Awali (Orientation) na  kufundisha kwa vitendo kwa kutumia vifaa vya kwenye mazingira yanayowazunguka ili wanafunzi waweze kuwaelewa na kupenda masomo. Mafunzo hayo yalipewa jina la Connected Learning for Secondary Schools STEM Teacher’s Capacity Builng (CL4STEM).

Aprili 29 – 30, 2024 Dkt. Edephonce Nfuka akiwa na Wataalamu wengine aliongoza ziara ya kutembelea walimu katika shule zote Tisa zilizoshiriki mafunzo hayo na kufanya tathimini kwa kile walichojifunza kama wanafunzi waweze kupenda masomo ya Sayansi.

Siku ya Kwanza Aprili 29, 2024 ziara ilianza katika shule za Sekondari Mgama iliyopo katika Kata ya Mgama, Tanangozi iliyopo katika Kata ya Mseke, Lipuli iliyopo katika Kata ya Kalenga na Bread of Life iliyopo katika Kata ya Kiwele.

Dkt. Nfuka ameweza kuona wanafunzi wakipenda masomo hayo kwa kuingia darasani wakati Mwalimu akiwa anafundisha, na kuona wanafunzi wanavyoshirikishwa katika ujifunzaji.

Aidha Dkt. Nfuka aliweza kuonana na Walimu wa masomo hayo na kujifunza juu ya changamoto na mafanikio waliyopata baada ya kufanya mapinduzi katika masomo hayo.

Walimu wameweza kutoa changamoto na mafanikio ambayo ilionesha mafanikio ni makubwa zaidi kuliko changamoto. Kwamba Mwalimu anaweza kutumia zana kutoka katika mazingira yanayowazunguka kuliko hapo awali, na pia wanafunzi wamebadilika sana kwa kupenda na kuyafurahia masomo hayo.

Siku ya Pili ambayo ilikuwa ni Aprili 30, 2024, ziara iliendelea katika Shule za Sekondari za Kibena Kata ya Ifunda, St. Mary’s, Lumuli Kata ya Lumuli, Shule ya Ufundi Ifunda na Shule ya Sekondari Lyandeembele Kata ya Ifunda.

Huko Dkt. Nfuka aliweza kujionea Walimu walivyofurahishwa na mafunzo waliyopata, na walimu wanaweza kushirikisha wanafunzi katika ufundishaji na ujifunzaji, pia ameweza kusisitiza walimu kutumia program hii na njia mbalimbali kwa ajili ya kujifunza zaidi.

Dkt. Nfuka amefurahishwa na mapokeo ya Walimu na Wanafunzi kwani Serikali itaweza kutafuta mbinu nzuri zaidi za kuwewezesha Walimu.  

Naye Afisa Taaluma wa Halmashauri Bi. Tina Sanga amewaambia walimu wasiache kutumia mbinu hizi kwani ni muhimu sana kwa uboreshaji wa taaluma, pia imemfanya mwalimu ajivunie kuwepo darasani kufundisha kifua mbele kwani mwanafunzi anamuelewa zaidi na hatimaye kuleta mabadiliko katika elimu.

Baadhi ya Walimu wamesema “katika mafunzo tuliyojengewa uwezo, tumeweza kujifunza zaidi ya kile tulichokuwa nacho, hii imetusaidia kuongeza ubunifu na kumshirikisha mwanafunzi kila hatua katika ujifunzaji, na kwamba mwanafunzi anelewa kwa haraka na kulipenda somo”.

Kadhalika Walimu wametoa maombi kwa Serikali kuwa, mafunzo kama hayo yawe yanatokea mara kwa mara, kwani inasaidia kuwakumbusha taaluma zao na kuwafanya wanafunzi wawepo muda wote wa vipindi.

Pia wameomba kuongezewa vifaa vya kisasa zaidi ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi zaidi, japo kwa sasa wamweza kutumia vishikwambi, kompyuta, na simu vinavyowasaidia kutufuta mbinu zaidi za ufundishaji.

 

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa