• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

CMT Iringa DC Yampongeza Mhe. Moyo kwa Utumishi wake

Imewekwa : February 3rd, 2023

CMT Iringa DC Yampongeza Mhe. Moyo kwa Utumishi wake

Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Iringa ambae kwa sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Nachwingea Mhe. Mohammed Moyo amekutana na kupeana salamu za mwisho na Mkurugenzi Mtendaji, Wakuu wa Idara na Vitengo Halmashauri ya Wilaya Iringa (CMT).

Katika kikao hicho kilichofanyika katika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji - Kalenga Wakuu wa Idara na Vitengo wamepata nafasi ya kumshukuru Mhe. Moyo kwa kipindi chote alichohudumu kama Muwakilishi wa Rais katika Wilaya ya Iringa, kumshukuru na kumpongeza kwa uchapakazi wake, ustaarabu na namna alivyotumia njia shirikishi katika uongozi wake.

Akizungumza katika kikao hiko kifupi Mkurugenzi Mtendaji Wakili Muhoja amesema anamshukuru na kumpongeza Mhe. Moyo kwani alikuwa akiwapa nafasi na kuwasikiliza Wataalamu wanasema nini na amekuwa akikubali kushauriwa na Wataalamu.

“kiukweli hata kwenye Halmashauri nyingine huko MaDC na MaDED hawasikilizani lakini kwako imekuwa tofauti, tulipata DC ambaye ni muelewa kama wewe kazi ilikuwa na amani”.

Umefanya mengi sana pia katika miradi nakumbuka hata kipindi cha madarasa 94 ziara zile ambazo tulipangiana napita huku, Mwenyekiti anapita kule na wewe unapita kule kwa kweli ilitusaidia sana na hiyo ilikuwa timu ya ushindi ambayo kila mtu angetamani kuwa nayo. Ameongeza.

Aidha amesema Mhe. Moyo amekuwa kiongozi mwema ambaye aliunganisha Chama, Serikali kwa maana ya Halmashauri na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, pia ameahidi yale yote aliyoyaanzisha basi yataendelezwa na Mkuu wa Wilaya Mpya.

Naye Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Bibi Lucy Nyalu amesema Mhe. Moyo amekuwa mchapakazi ameweza kufika katika vijiji vyote na amekuwa mtu wa kuomba ushauri kabla ya kuchukua maamuzi na pia amemuomba kama kuna sehemu ambayo walikwazana basi Mhe. Moyo awasamehe.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Ardhi Ndugu Geofrey Kalua amesema yale yote mema na mazuri aliyoyaacha Mhe. Moyo basi yataendelezwa.

Akizipokea salamu, shukrani na pongezi hizo Mhe. Moyo amewashukuru pia Wakuu wa Idara na Vitengo kwa ushirikiano na amesema kuwa alipochaguliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Iringa alikuwa mgeni sana katika masuala ya Serikali lakini kufanikiwa kwake hasa katika ziara zake ni kutokana na Wakuu wa Idara kwa sababu walimfunza na kumshauri nini cha kufanya.

“yale mazuri yangu mtayachukua na yale mabaya yangu niachieni mwenyewe niende nayo, lakini kufanikiwa kwangu mpaka Mhe. Rais kuniona niendelee ni kutokana na nyie, mmesababisha nionekane nafaa”.

Ninajua tumefanya kazi vizuri na ndio maaana nikamuomba Bashir angalau tuagane, sisi ni binadamu huenda tulikwazana lakini nyie hakuna mtu alionikwaza ninaondoka kwa furaha kwa sababu mmenifunza mengi. Amesema.

Kadhalika amewaasa pia Wakuu wa Idara kumpatia ushirikiano wa kutosha Mkuu wa Wilaya Mpya na kusaidiana katika miradi mikubwa ya maendeleo kama skimu ya umwagiliaji ya Mkombozi nakadharika.

Mhe. Moyo kwa sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea inayopatikana Mkoani Lindi na kwa sasa Wilaya ya Iringa inaongozwa na Mhe. Veronica Kessy.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa