• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

CMT Yafanya Ziara Kukagua Miradi ya Maendeleo ya Kwa Robo ya Kwanza 2022/2023

Imewekwa : October 20th, 2022

Kamati ya Menejiment Yafanya Ziara

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Daktari Samwel Marwa ameongoza Kamati ya Menejimenti kufanya ziara kukagua miradi ya maendeleo kwa kipindi cha Robo ya Kwanza kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 tarehe 17/10/2022

Katika ziara hiyo Kamati imetembelea baadhi ya Kata za Halmashauri zikiwemo Kata ya Kihorogota katika Kijiji cha Mikongw’i kwenye mradi wa ujenzi wa vyoo matundu saba ya Zahanati.

Mradi huo wa vyoo vya Zahanati umekadiriwa kutumia kiasi cha Shilingi Milioni 28.4 ambapo kati ya hizo kiasi cha shilingi Milioni 4.2 ni nguvu za wananchi. Ujenzi ulianza tarehe 05/08/2022 na unategemewa kukamilika tarehe 05/11/2022 hadi sasa ujenzi umefikia 35/%, ujenzi unaendelea.

Kamati iliendelea na ziara yake hadi Kata ya Kising’a Kijiji cha Kinywang’anga kwenye mradi wa ujenzi wa Zahanti, ambapo mradi unakadiriwa kutumia kiasi cha Shilingi Milioni 50.

Ujenzi wa Zahanati hiyo ulianza mwezi Aprili 2022 na ulitegemewa kukamilika mwezi Agosti 2022, ambapo kutokana na changamoto zilizo nje ya uwezo, haukuweza kukamilika kwa wakati. Ujenzi umefikia 99% ambapo hatua ya ufungaji wa mabomba ya maji unaendelea.

Kamati pia imeendelea kufanya ziara katika Kata ya Kiwele Kijiji cha Kitapilimwa kwenye ujenzi wa Kituo cha Afya na kukagua baadhi ya majengo ambayo yanaendelea na ujenzi, ambapo ni ujenzi wa wodi ya wazazi na upasuaji, jengo la kufulia nguo na kichomea taka. Majengo mengine ya OPD na maabara yalikwishakamilika, na yametumia kiasi cha Shilingi Milioni 250. Ujenzi umefikia 60% na ujenzi bado unaendelea.

Mwenyekiti ameendelea kuongoza Kamati na kwenda Kata ya Itunundu katika Hospitali ya Wilaya Igodikafu ambapo kuna ujenzi wa jengo la dharura lililotumia kiasi cha Shilingi Milioni 300 kwa fedha za UVIKO-19, nyumba ya mtumishi mbili kwa moja (2 in 1), ambapo zimetumika kiasi cha Shilingi Milioni 90, wodi ya upasuaji kwa wanawake na wodi ya upasuaji kwa wanaume, jengo la kuhifadhia maiti na jengo la upasuaji (Main Theatre), ambapo zimetumika kiasi cha Shilingi Milioni 800.

Kamati pia imefanya ziara katika Kata ya Mlenge Kijiji cha Magombwe ambapo kuna mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Mlenge. Mradi huu umeletwa na Serikali kupitia progamu ya Secondary Education Quality Improvement Programme (SEQUIP) kwa fedha za Benki ya Dunia (World Bank), ambapo kiasi cha Shilingi Milioni 600 zimetolewa kukamilisha mradi huu, lakini awamu ya kwanza zimetolewa kiasi cha Shilingi Milioni 470 ili kuanza mradi. Katika kiasi hicho yamejengwa madarasa nane (8), maabara tatu (3), jengo la Utawala, Maktaba, chumba cha TEHAMA, vyoo vya wanafunzi wa kike na wa kiume matundu kumi na nane (18), vyoo vya Walimu.

Katika awamu hiyo ya fedha madarasa manne (4) yamekamilika kwa 100% ujenzi wote kwa ujumla umefikia 75%. Ujenzi bado unaendelea.

Mwenyekiti ametoa rai kwa Mkandarasi anayetekeleza mradi huo kuongeza kasi ya ujenzi kwani majengo hayo yanategemewa kuanza kwa watoto wa Kidato cha Kwanza 2023. Kutokana na majengo mengine kutokamilika kwa wakati kiasi cha Shilingi 214.5 zinahitajika.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa