• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC IRINGA MHE. KHERI JAMESI AFANYA ZIARA YA KIKAZI TARAFA YA ISIMANI IRINGA DC

Imewekwa : March 22nd, 2024


Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Kheri James amefanya ziara katika Tarafa ya Isimani Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Machi 22, 2024 ambapo amepata fursa ya kuongea na watumishi pamoja na wananchi.

Akizungumza na wananchi wa Isimani Mhe. Kheri Jamesi amesema kuwa lengo la serikali ni kuboresha mazingira ya wananchi kufanyia kazi ili kujiingizia kipato “Tumepokea fedha kwenye afya, maji, barabara, tumepokea fedha nyingi sana kwenye skimu za umwagiliaji, tumepokea fedha katika elimu, na kwa kweli kila mtu anashuhudia maana hakuna kata ambayo haijaguswa na mguso wa maendeleo lakini haya yote ambayo Mhe. Rais anayafanya anayafanya kwa faida ya mimi na wewe” amesema Mhe. Kheri.

Aidha, Mhe. Kheri ametoa pongezi zake kwa kazi kubwa inayofanywa na Halmashauri kwenye utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo na kutambua uwepo wa wataalamu wa idara mbalimbali zikiwemo, kilimo na elimu chini ya Mkurugenzi Mtendaji ndg. Robert Masunya.

Kuhusu suala la lishe na utoaji wa chakula mashuleni, Mhe. Kheri amewaasa viongozi ambao vijiji vyao vina miradi inayoingiza mapato, watenge kiasi cha fedha kwa ajili ya chakula cha wanafunzi shuleni. Pia amewataka viongozi wa vijiji na kata kutumia mbinu rafiki kuwafanya watu waelewe na kuchangia chakula cha wanafunzi shuleni.

Mhe. Kheri pia amepata nafasi ya kuwasikiliza wananchi ambapo ametoa maelekezo kuhusu magari ya kubebea wagonjwa na kusema kuwa hakuna kuchangisha wananchi fedha kwa ajili ya mafuta ya gari ya kubebea wagonjwa wala fedha za kufanyia matengenezo kwani serikali inayahudumia magari hayo.

Kwa upande mwingine Mhe. Kheri ametoa maelekezo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kuweka utaratibu wa vijiji kuwa kwenye mpango wa matumizi bora ya ardhi ili kuepuka migogoro mbalimbali ya ardhi ikiwemo migogoro baina ya wakulima na wafugaji.

Nao wananchi wa tarafa ya Isimani wameishukuru Serikali ya Awamu ya sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapelekea miradi ambayo imekuwa msaada mkubwa sana kwao ikiwemo miradi ya maji.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa