• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC Kessy Afanya Ziara kwa Siku Mbili Kukagua Miradi ya Maendeleo

Imewekwa : May 14th, 2023

DC KESSY AKAGUA MIRADI NA KUZUNGUMZA NA BARAZA LA MAENDELEO LA TARAFA YA KIPONZELO NA ISIMANI

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Veronica Kessy amefanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya Maendeleo katika Tarafa ya Kiponzelo, Kalenga na Isimani.

Ziara hiyo ambayo imekuwa ya siku mbili tarehe 12-13/05.2023, Mhe. Kessy amepata fursa ya kuzungumza na Wajumbe wa Kamati za Maendeleo Tarafa ya Kalenga na Isimani kwa lengo la kujitambulisha na kusikiliza kero kutoka kwa wajumbe wa maeneo husika

Miradi iliyotembelewa na kukaguliwa ni pamoja na ujenzi wa nyumba ya walimu ya familia mbili (two in one) katika Shule ya Msingi Kihanga, ambapo Serikali imepeleka Kiasi cha Tsh. 50,000,000/- kwaajili ya Umaliziaji wa kazi hiyo, umaliziaji wa Zahanati ya Kijiji cha Mwambao, Kata ya Ulanda ambapo pia Serikali Imepeleka fedha kiasi cha Tsh. 50,000,000/- za umaliziaji na ujenzi wa miundombinu ya vyoo, umaliziaji wa jengo la nyumba ya walimu katika shule ya Msingi Mlambalasi ambapo vilevile Serikali imepeleka kiasi cha Tsh. 50,000,000/- kwa ajili ya kazi hiyo, ujezi wa uzio na matundu ya vyoo katika Shule ya Msingi Kipera iliyopo Kata ya Nzuhi. Hii ni Shule Jumuishi ambayo ina watoto wenye ulemavu wa aina mbalimbali yaani wasioona, viziwi, wenye ulemavu wa ngozi, wenye ulemavu wa viungo, usonji na ulemavu wa akili. Katika shule hii Serikali imepeleka kiasi cha Tsh. 30,000,000/- kwaajili ya ujenzi wa uzio na matundu ya vyoo na kazi imeshaanza, umaliziaji wa nyumba ya Walimu katika shule ya Msingi Mikong’wi ambapo kazi ipo katika hatua ya umaliziaji. Hapa Serikali imetoa kiasi cha Tsh. 25,000,000/- na kazi inaendelea, umaliziaji wa jengo la Zahanati katika Kijiji cha Holo ambapo Serikali imepeleka Fedha Zaidi ya Tsh. 51,000,000/- ili kufanya umaliziaji wa upande mmoja wa Zahanati ambao utaanza kutumika kutolea huduma kwa wananchi. Miradi hii yote imeanza kufanyika katika Mwaka wa Fedha 2022/2023.

Aidha, Mhe. Kessy alipata fursa ya kuwatembelea wanakikundi cha ufugaji wa mbuzi katika kijiji cha Makatapola Kata ya Izazi, ambao Serikali imewawezesha kuanzisha mradi huo ikiwa na lengo la uhifadhi wa mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji na Serikali kupitia ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira kwa awamu ya kwanza imetumia Zaidi ya Tsh. Milioni 188 kwenye kuwezesha vikundi.

Mh. Kessy amewasisitiza wananchi kutumia miradi hii kama fursa na kwamba wanatakiwa kuitunza na kuilinda ili iweze kudumu kwa vizazi vijavyo.

Kwa upande wao, wananchi pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali na Chama Cha Mapinduzi wametoa pongezi zao za dhati kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali ya Awamu ya Sita kwa kutoa fedha nyingi za miradi mbalimbali ya Maendeleo.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa