• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC Kessy Akemea Vikali Wizi wa Mita za Maji

Imewekwa : September 6th, 2023

“Natoa Siku Saba Mita za Maji Zilizoibiwa Zirudishwe” – DC Kessy

Wananchi wa Kijiji cha Kiponzero Kata ya Maboga wamepewa siku saba kurudisha mita za maji zilizoibiwa katika mabomba mbalimbali, kufuatia mgogoro uliopo kati ya wananchi na Mwenyekiti wa Kijiji hicho ambapo wananchi hawataki kulipia huduma za maji.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Veronica Kessy alipokwenda kutatua mgogoro kati ya wananchi na Mwenyekiti wa Kijiji cha Kiponzero Ndugu Allen Exavery Dallu siku ya Jumatano tarehe 06/09/2023

“wananchi mnafanya kosa kubwa kuiba mita za maji na kumuondoa Mwenyekiti wa Kijiji madarakani, kwa madai yenu kuwa hamumuhitaji bila sababu za msingi. Inatakiwa mfuate sheria, kanuni na taratibu kwani Mwenyekiti huyo amekuwepo kwa sheria na taratibu. Kuazia sasa natoa siku saba mita za maji zirudishwe na walioiba mita hizo watachukuliwa hatua, pia Mwenyekiti bado yupo madarakani kama kawaida”.

Aidha Mheshimiwa Kessy amesisitiza suala la kulinda mazingira na kutunza vyanzo vya maji kwa kufanya usafi na kupandi miti kwa wingi ambayo ni rafiki wa maji. Pia suala la lishe limkuwa tatizo katika jamii ya Iringa na kuongeza kusema kuwa, ni muhimu kupanda miti ya matunda na kuwapatia watoto mlo kamili ili kuondokana na udumavu.

Naye Mwanasheria wa Halmashauri Bi. Stella Makali aliwasomea wananchi sheria na taratibu zinazopaswa kufuatwa endapo kunakuwa na tatizo kama hilo.

Naye Meneja wa Mamlaka ya Maji Vijijini (RUWASA) Mhandisi Exaud Humbo amesema, “mwananchi anatakiwa kuchangia huduma za maji ili kwamba miundombinu ikiharibika inakuwa rahisi kutumia pesa zilizochangiwa kurekebisha”.

Mhandisi Humbo ameendelea kusema kuwa, “miundombinu ya kijiji hiki ni ya muda mrefu hiyo kutotosheleza mahitaji ya maji kwa wananchi kwa wakati mmoja. Serikali imeleta kiasi cha Shilingi Bilioni 4 kwa ajili ya kujenga upya miundombinu ya maji ambayo itakuwa mkombozi kwa kero za maji. Michoro ipo tayari kilichobaki ni kuanza kazi tu”

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Komredi Costantine Kihwele alikuwa na haya ya kusema “Serikali ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan inatoa fedha nyingi kutekeleza miradi mbalimbali kwa ajili ya wananchi wake. Lakini ninyi mnaharibu miundombinu ambayo ipo kwa faida yenu, jambo hili haliwezi kufumbiwa macho. Ninyi wananchi mnatakiwa kuwa wa kwanza katika kulinda rasilimali hizi kwa ajili ya vizazi vyenu.

Wananchi walipata nafasi ya kutoa kero zao mbalimbali, ikiwemo ubovu wa miundombinu ya barabara. Mheshimiwa Kessy alichukua kero zao na kuahidi kufanyika kazi hivi punde.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa