• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC Kessy Aongoza Kikao cha Tathimini ya Mkataba wa Lishe

Imewekwa : November 15th, 2023

DC Kessy Aongoza Kikao cha Tathmini ya Mkataba wa Lishe Robo ya Kwanza

“Mama akiwa na mimba ya siku moja, lazima tuanze kumtengeneza ili mama na mtoto wasipate udumavu”.

Kauli hii imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Veronica Kessy, alipokuwa anafungua kikao cha Tathmini ya Mkataba wa Lishe Wilaya kwa Robo ya Kwanza (Julai – Septemba). Kikao hicho kimefanyika leo Novemba 15, 2023 katika Ukumbi wa Halmashauri uliopo Ihemi Kata ya Mgama.

Mheshimiwa Kessy ameongeza kusema kuwa, Rais wa Awamu ya Sita Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amesema Mikoa yote yenye udumavu ijitathamini. Hii ni kutokana na Mkoa wa Iringa kuwa na wadumuvu.

“Tunatakiwa kuwa wabunifu katika suala la kutokomeza udumavu, kwani akina mama tunakaa na watoto muda mwingi hivyo tunawajibika katika malezi na makuzi ya mtoto”. Mkoa wa Iringa haustahili kuwa na udumavu kutokana na wananchi wake kuzalisha vyakula mbalimbali na matunda kwa wingi sana”.

Mheshimiwa Kessy amegusia suala la unywaji wa pombe na uvutaji wa sigara kwa mama mjamzito pia sababu kubwa inayochangua udumavu.

Pamoja na hayo Mheshimiwa Kessy ametoa agizo kwa Watendaji wa Kata wote kuwa, kila Mtendaji atengeneze shamba darasa, na kushirikisha wananchi ili waje wajifunze hapo, na kila mmoja achukue hatu ili kuleta matokeo chanya.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Stephen Mhapa amesema, Watendaji wasijitetee kuhusu utafiti unaofanywa na Sekta binafsi, wanatakiwa wafanye kazi bila kuangalia nani kafanya nini. Pia amewatia moyo kwa kazi nzuri wanazofanya na kuwahimiza Watendaji hao waendelee kutoa elimu kwa wananchi juu ya madhara ya udumavu, kwani kuna baadhi ya changamoto haziepukiki.

Akitoa taarifa ya Kadi Alama ya utekelezaji wa viashiria vya Mkataba wa Lishe Ngazi ya Wilaya kwa kipindi cha Julai –Septemba Afisa Lishe Wilaya Bi. Tiliza Mbulla amesema “lishe imeendelea kujadiliwa kwa kuzingatia mkakati wa lishe wa Kitaifa ili kuweza kufanikisha matokeo tarajiwa, kupunguza lishe duni, kupunguza ukosefu wa virutubishi, kupunguza uzito uliozidi na uliokithiri na kuweka mazingira wezeshi ya lishe. Hivyo ili kuhakikisha matokeo tarajiwa yanafikiwa utekelezaji unafanyika na kupimwa kuptia viashiria vya mkataba wa lishe”.

Bi. Tiliza ameendelea kusema, utekelezaji wa utoaji wa chakula shuleni unaoratibiwa na Watendaji wa Kata umeendelea kuimarika ambpo Kata moya ya Ilolompya ndiyo yenye idadi ndogo ya wananfunzi wanaopta walau mlo mmoja.

Aidha, katika kiashiria cha kiasi cha fedha zilizotumika kwa kila mtoto wa umri chini ya miaka mitano katika Halmashauri (Tsh. 1,000.00) na asilimia ya fedha zilizotumika kutekeleza shughuli za lishe zilitolewa kwa asilimia 106 kulingana na mpango. Pia wazazi na walezi waliohudhuriia kliniki ya afya ya uzazi na mtoto walipata elimu ya ulishaji wa watoto wachanga na wadogo ambapo ilifikiwa kwa asilimia 100.

Bi. Tiliza ameendelea kwa kubainisha mafanikio katika kutekeleza viashiria vyote vya Mkataba kwa ufanisi na ongezeko la asilimia 2.0 kwa idadi ya shule zinazotekeleza mpango wa utoaji chakula shuleni.

Pia changamoto ya uchangiaji usioridhisha wa chakula kwa wananfunzi pamoja na kutopatikana kwa vyakula vilivyoongezwa virutubisho, na kuweza kutatua changamoto hiyo kwa kuendelea kutumia majukwaa mbalimbali kuelimsha jamii juu ya umuhimu wa uchangiaji chakula, na kuanzisha mashamba ya shule.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa