• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC Moyo Aagiza Elimu Itolewa Kuhusu Chanjo ya Matone ya Ugonjwa wa Polio

Imewekwa : November 29th, 2022

DC Moyo Aagiza Elimu Itolewa Kuhusu Chanjo ya Matone ya Ugonjwa wa Polio

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Mohammed Moyo ameitaka Kamati ya Msingi ya Afya ya Jamii kuendelea kutoa elimu kuhusu ugonjwa wa polio kwa wananchi wote na kuwaelezea umuhimu wa chanjo hiyo kupitia majukwaa mbalimbali zikiwemo Taasisi wanazofanyia kazi.

Aidha amewataka kutoa taarifa za utekelezaji wa kampeni katika ngazi mbalimbali ikiwemo kusimamia shughuli zote za kampeni katika eneo au Taasisi zao.

Ameyasema hayo mapema leo Novemba 29, 2022 katika kikao cha Kamati ya Msingi ya Afya ya Jamii kilichofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kikiwa na lengo la kutoa mafunzo kwa kamati hiyo

“Lengo la kampeni hii ni kuwa mabalozi wa kuendesha kampeni dhidi ya ugonjwa huu hatari wa Polio kwa kuhamasisha watoto wote katika jamii zetu walio chini ya miaka mitano wapatiwe chanjo ya Matone ya Polio.”

Aidha nawasisitiza mkaendelee kuihamasisha kampeni hii ili iweze kufanikiwa, Hapa Mwenyekiti wa Halmashauri upo katika majukwaa au vikao vyako huko basi pia utumie fursa hiyo kuhamasisha kampeni hii ya Chanjo ya Matone ya Polio. Ameongeza.

Naye Mkuu wa Idara ya Afya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Dokta Samwel Marwa amewahakikishia kuhusu usalama wa chanjo ya polio kuwa haina madhara yoyote hivyo ni salama kwa watoto na ikiingia mwilini hutoka kwa njia ya haja ndogo, kubwa au kucheua.

“Ninapenda kuwahakikishia  tu kuwa chanjo hii inatumiwa na inafanya kazi vizuri zaidi kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano na haina changamoto yoyote.” Amesema.

Akitoa ufafanuzi wa chanjo ya polio Mratibu wa Huduma za Chanjo Wilaya Ndugu Sospeter Tiyara amesema polio ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vya polio, Ugonjwa huu unapelekea kupooza na hatimaye kifo na amesema ugonjwa wa polio hauna tiba lakini unaweza kuzuiliwa kwa kupata chanjo ya matone ya polio.

“kwa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa imetekeleza utoaji wa chanjo ya polio ya matone kwa awamu 2, kwa maana ya awamu ya pili na tatu kwa nchi nzima. Awamu ya pili walengwa walikuwa  47,158 waliochanjwa 51646 sawa na asilimia 110% na awamu ya tatu walengwa walikuwa ni 53,191 Waliochanjwa 55,055 sawa na asilimia 103.50”.

Mratibu wa Chanjo Ndugu Tiyara amesema chanjo ya polio ya matone awamu ya tatu itafanyika Tanzania Bara pamoja na Zanzibar na kampeni hiyo itaanza rasmi tarehe 01 hadi 04 Disemba 2022 na wahamasihaji wataanza shughuli za uhamasishaji siku mbili kabla ya kuanza kampeni na kampeni hizi zitafanyika nyumba kwa nyumba na maeneo mengine kuhakikisha watoto wote walengwa wanafikiwa.

Sambamba na uchanjaji huduma zingine ziatatolewa ikiwemo elimu ya chanjo, kuimarisha huduma za chanjo katika vituo vya kutolea chanjo pamoja na kuwatafuta na kuwafatilia watoto wote wenye umri chini ya miaka kumi na tano ambao wamepata ulemavu wa ghafla tepetepe (washukiwa wa ugonjwa wa polio) na kutoa taarifa katika vituo vya karibu kwa uchunguzi na kubaini ugonjwa huu wa polio.

   

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa