• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Halmashauri Kuu ya CCM Yafurahishwa na Utekelezaji wa Ilani

Imewekwa : September 8th, 2023

Halmashauri Kuu ya CCM Yafurahishwa na Utekelezaji wa Ilani

Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), imefurahishwa na utakelezaji mzuri wa Ilani kwa kusimamia miradi mbalimbali katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Mkutano huo umefanyika Septemba 07, 2023, katika Ukumbi wa Halmashauri wa Siasa ni Kilimo.

Akiongea katika hotuba yake fupi katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya Komredi Costantine Kihwele amesema “kuna mtu ametokea CCM na kuna mtu amepitia CCM, hawa ni watu wawili tofauti.  Namaanisha kuwa, huyu Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Veronica Kessy ametokea CCM, hivyo nampongeza kwa utekelezaji mzuri wa Ilani katika kusimamia miradi mbalimbali. Amenipa ushirikiano wa kutosha kwa kila jambo, hivyo nampongeza sana”.

Aidha Ndugu Kihwele amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja na Menejimenti yake kwa ujumla kwa usimamizi mzuri na wa uwazi katika kusimamia miradi ya Halmashauri.

Komredi Kihwele ameweza kutoa Hati za Pongezi kwa Madiwani 38 wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa wakiwemo wa Vita Maalum na Wabunge, wa Jimbo la Isimani Mheshimiwa William Lukuvi na wa Jimbo la Kalenga Mheshimiwa Jackson Kiswaga.

“Kwa kasi hii ya utekelezaji wa Ilani hatuna cha kumlipa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan zaidi ya kumuahidi ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika 2024”.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa Ilani katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2022/2023 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Veronica Kessy ameweza kuzungumzia wingi wa watu kwa mujibu wa Sensa ya mwaka 2022 Halmashauri ina jumla ya watu 315,354  ikiwemo wanawake 161,798.

Pia ameweza kugusia hali ya watumishi na stahiki zao mbalimbali za kiutumishi na mambo mengine ya ukusanyaji wa mapato ya ndani kuwa, hadi kufikia Juni 2023 zaidi ya kiasi cha Shilingi Bilioni 3.9 sawa na asilimia 99 ya makadirio ya bajeti ya mwaka zilikusanywa. Maendeleo makubwa ya huduma za elimu, maji, afya, barabara, umeme, uboreshaji wa kazi za Mamlaka za Serikali za Mitaa na hali ya usalama katika Halmashauri.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Wakili Bashir Muhoja amesema, “nikiangalia timu yangu naona waliotoka ndani ya Iringa ni wachache, hivyo wengi tumetoka mbali na kuja kuhudumia wananchi wa Iringa. Uwepo na changamoto ni kawaida kwani penye mafanikio hapakosi changamoto, na kwamba tunazichukua kama fursa. Japo hatutaweza kwa asilimia 100 lakni tunajitahidi kwa kadiri ya uwezo wetu”.

Wakili Muhoja ameendelea kuseama kuwa, “watumishi wapo tayati kutekeleza Ilani hasa kwa kipindi hiki kabla ya uchaguzi. Tunashukuru kwa kuendelea kutusimamia na kutukosoa pale tunapokosea katika utendaji wetu wa kazi”

“Bado siku chache Darasa la Saba wafanye mitihani yao ya kuhitimu elimu ya msingi, ambapo itafanyika tarehe 13 -14 Septemba, 2023, hivyo tuwaombee”.

Kadhalika Wakili Muhoja ameongeza kusema kuwa, Hospitali ya Wilaya iliyopo Igodikafu imeanza kutoa huduma za upasuaji, na kwamba hivi karibuni tutapokea gari ya wagonjwa ili kurahisisha huduma.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa