• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Hatujakatazwa kuendeleza Mila Ambazo ni Nzuri na Rafiki - RC Dendego

Imewekwa : November 27th, 2022

Hatujakatazwa kuendeleza Mila Ambazo ni Nzuri na Rafiki - RC Dendego

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Halima Dendego amewataka Viongozi wa kidini, Kimila pamoja na Watanzania wote kurudisha na kuendelea kuzidumisha mila zetu kuanzia kwenye ngazi ya familia (malezi),  shule pamoja na katika maisha ya kila siku.

Amesema Wazazi ni lazima kusema na watoto ikiwemo kuwakanya wanapokosea na sio kuwacha kutumia muda mwingi katika mitandao ya kijamii kwani huko ndiko wanakoharibiwa na kuzalisha makatili wa sasa na baadae.

Ameyatamka hayo katika uzunduzi wa Kampeni ya Siku Kumi na Sita za Kupinga Ukatili wa Kijinsia na Watoto uliofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa (Siasa ni Kilimo) na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Mkoa na Wilaya zote.

"Matukio ya kikatili yanaumiza, yanaumiza akili na yanaumiza mwili wakati mwingine kabisa yanapelekea baadhi ya watu kuwa na msongo wa mawazo na mwisho kupotelea huko".

Amesema pia katika siku hizi kumi na sita za kupinga ukatili amepanga kupita katika shule zote akiwa na Waandishi wa Habari kusisitiza kuhusu kutoa adhabu kwa wanafunzi pale wanapokosea.

"Sasa hivi wazazi tunawaogopa watoto, tunaona wanaharibika lakini tunaogopa kusema nao, wanashindwa kutueleza wanapokutana na dalili za ukatili kwa sababu hatujawajengea uwezo wa kukabiliana na viashiria fulani vya ukatili".

Aidha amesema vitendo hivi vya kikatili vimekuwa vikifanywa na watu wa karibu wakiwemo ndugu na kwa sababu wazazi hawapatikani nyumbani wanakuwa katika shughuli za utafutaji basi wajomba, baba wadogo na ndugu wengine hutumia mwanya huo kufanya vitendo hivyo vichafu.

"Na leo vitendo vingi vunafanyika nyumbani na watu wa karibu ambao wazazi wamewakaribisha na wanatumia nafasi hiyo kubaka, kulawiti watoto wetu".

Kadhalika amelitaka Jeshi la Polisi Mkoa Wa Iringa kuhakikisha ndani ya hizi siku kumi na sita wanakamilisha upelelezi wa mashauri yote ya ukatili ambayo yameripotiwa yaweze kukamilika na kushughulikiwa kulingana na sheria ili iweze kuwa mfano kwa jamii.

Naye Katibu Tawala Mkoa Mhandisi Leonard Robert Masanja amesema dhana ya ukatili ni pana sana na imekua ikianzia katika ngazi ya familia hivyo amewataka watu wote kuanza kupigana vita hivi na amesena itakua vyema kama itaanzia damuni yani kwa kuvichukia vitendo hivo.

"Matukio haya yanakwenda mbali zaidi mpaka mashuleni walimu wamekua wakibaka wanafunzi, hata Vyuoni pia wanawake wamekua wanyanyaswa kingono ili waweze kufaulu mitihani kadhalika Maofisini Wanawake wamekuwa wakiombwa Rushwa ya ngono ili wapate kazi hii haikubaliki". Amesema.

Ufunguzi wa Kampeni hizi umefunguliwa rasmi Novemba 25, 2022 na kutamatika Disemba 10 ikiwa na kauli mbiu isemayo "Kila Uhai Una thamani Tokomeza ukatili wa wanawake na watoto".





Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa