• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Iringa DC Kuimarisha kikosi kazi Usimamzi na Ukusanyaji Mapato

Imewekwa : October 19th, 2022

Iringa DC Kuimarisha kikosi kazi Usimamzi na Ukusanyaji Mapato 

Halmashauri za Mkoa wa Iringa zimekutana kwa lengo la kujadili taarifa za utekelezaji wa shughuli za Mamlaka ya Serikali za Mitaa kwa robo ya kwanza (julai hadi septemba) mwaka wa fedha 2022/2023. Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kwa siku mbili tarehe 18 na 19.10.2022.

Katika mwaka wa fedha 2022/23, Halmashauri za Mkoa ziliidhinishiwa kukusanya jumla ya shilingi 26,744,971,245.32 kutoka katika vyanzo vyake vya ndani (Own Source). Hadi kufikia tarehe 30 septemba, 2022 jumla shilingi 5,141,808,845.32 zilikuwa zimekusanywa sawa na asilimia 19.22 ya lengo.

Mchanganuo wa makusanyo ya ndani kwa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kwa kipindi cha kuanzia tarehe 01 julai, 2022 hadi tarehe 30 septemba, 2022 bajeti iliyoidhinishwa ni Tshs. 4,269,100,000.32 na makusanyo hadi kufikia tarehe 30 septemba 2022 ni 720,321,648.00 na jumla ya asilimia ya makusanyo ni 17.00.

Akiwasilisha mafanikio yaliyopatikana wakati wa ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa robo ya kwanza mwaka wa fedha 2022/2023 Mchumi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Fredy Kaduma amesema wamefanikiwa kuanzisha vyanzo vipya vya mapato ambavyo ni nyumba mbili (2) apartment za kupangisha, ushuru wa maegesho wa magari na ushuru wa stendi ya basi - Migoli.

Kwa upande wa changamoto Kaduma amesema Halmashauri imekumbana na changamoto ya ukosefu wa soko la ununuzi wa zao la tumbaku, wakulima wameacha kuzalisha na hivyo Halmashauri kukosa mapato kwenye ushuru huu. Kadhalika kushuka kwa uzalishaji wa samaki katika bwawa la samaki la Mtera limeathiri kiwango cha ukusanyaji mapato.

Utambulisho wa vitambulisho vya Ujasiriamali pia vimepunguza mapato yaliyokuwa yakikusanywa kwenye baadhi ya vyanzo ambavyo Halmashauri inavitegemea kwa kuwa na mchango mkubwa kwenye bajeti ya mapato ya ndani ikiwa ni eneo la makusanyo ya ushuru wa mazao/mbogamboga na matunda. Ameongeza.

Amesema hatua zilizochukuliwa na Halmashauri kukabiliana na changamoto hizo ni pamoja na Halmashauri imeandaa mfumo wa kanzidata (database) ili kuorodhesha walipa kodi wote wa ushuru mbalimbali wa Halmashauri kadhalika na kuendelea kuimarisha ukusanyaji wa mapato kwa njia ya kielektroniki na kuimarisha kikosi kazi cha kusimamia na kukusanya mapato ya Halmashauri.

“Halmashauri pia imeendelea kufanya mawasiliano na wanunuzi wakubwa wa zao la tumbaku na kutataua changamoto zinazozikabili vyama vya msingi ili waweze kulima tena na Halmashauri ikusanye mapato.”    

Katibu Tawala Msaidizi Mkoa, Sehemu ya Mipango na Uratibu Ndugu Kasongwa Owden amesisitiza juu ya usimamizi na ufuatiliaji wa miradi na vyanzo mbalimbali vya mapato ili kuweza kufikia malengo yaliyowekwa kama makisio ya ukusanyaji wa mapato.

 Naye Muweka Hazina wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Bibi Jwani M. Yengi amesema kuwa kumekuwa na changamoto mbalimbali zinazokwamisha ukusanyaji wa mapato lakini nyingi katuika hizo zinafanyiwa kazi

 “Tunatarajia kuingiza kiasi cha Tshs. Milioni 400 kutoka katika chanzo cha uuzaji wa viwanja ili kufikia lengo tumeanza uhamasishaji kwa njia mbalimbali ikiwemo matangazo lakini pia tunatarajia kupunguza bei ili tuweze kufikia lengo lililowekwa”.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa