Halmashauri ya Wilaya ya Iringa mapema hii leo Aprili 29, 2025 imekabidhi Mwenge wa Uhuru 2025 katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo ukiwa umemaliza mbio zake Iringa DC kwa kukimbizwa kilometa 182.
Mwenge wa Uhuru 2025 katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa umepitia miradi 8 yenye thamani ya zaidi ya Bilioni 4.4 sanjari na klabu za mapambano dhidi ya madawa ya kulevya, rushwa, VVU/UKIMWI, Ukatili wa kijinsia na klabu ya lishe.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ndugu Ismail Ali Ussi amepongeza utekelezaji na ubora wa miradi mbalimbali iliyopitiwa na Mwenge huku akisisitiza vijana kuchangamkia fursa zinazotokana na mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri.
Ujumbe mkuu wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu unasema, "Jitokeze kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu"
@ikulu_mawasiliano
@ortamisemi @msemajimkuuwaserikali
@wizara_sanaatz
@iringarc
@iringa_district
@ndg.kheri_james
@am_54masunya_r
Kijiji cha Ihemi
Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa
Simu ya mezani: 026-2702828/2702585
Simu ya mkononi: 0757 364 994
Barua pepe: ded@iringadc.go.tz
Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa