• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Kamati ya Fedha Yampa Tano Muhoja,

Imewekwa : February 2nd, 2023

Kamati ya Fedha Yampa Tano Muhoja,

Mhapa Asema ni DED wa Kipekee

Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango Halmashauri ya Wilaya ya Iringa wametoa sifa na pongezi nyingi kwa Mkurugenzi Mtendaji Wakili Bashir Muhoja kwa namna anavyosimamia na kutekeleza miradi mbalimbali ya Halmashauri.

Wajumbe wa Kamati hiyo ambao ni Waheshimiwa Madiwani wameonesha mahaba yao wazi wazi ya namna walivyofurahishwa na kupendezwa na kwa jinsi Mkurugenzi Mtendaji anavyofanya kazi kwa bidii na juhudi kubwa huku akiitekeleza miradi kwa ubora wa hali ya juu.

Hayo yamejiri tarehe 2 Februari wakati Kamati hiyo ilipokua katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo namna ilivyotekelezwa na kufanya tathmini ya pamoja kama kamati mama.

Katika pongezi hizo wakiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Stephen Mhapa amesema kuwa Mkurugenzi Wakili Muhoja amekuwa kiongozi na mtendaji wa kipekee anaefanya kazi kwa ukaribu na Waheshimiwa Madiwani.

"Mimi nimefanya kazi na Wakurugenzi wengi sana lakini utendaji kazi wa Muhoja ni wa kipekee sana, yani ni mfuatiliaji na huo ndio ukweli".

Aidha amesema kuwa Muhoja amekuwa na maelezo ya kutosha kuhusu miradi yote inayotekelezwa bila kutegemea majibu kutoka kwa Wakuu wa Idara, huku akiifahamu miradi yote pamoja na matumizi ya fedha namna ilivyotumika.

"Mimi nasema nakupongeza sana Mkurugenzi, kazi tumeiona, madarasa, zahanati, vituo vya afya tumejenga na licha ya changamoto zote lakini umekua mvumilivu, Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, Mimi nakupongeza sana Muhoja".

Kadhalika Mhe. Mhapa amewapongeza wasaidizi wa Mkurugenzi yaani watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa na amesema mchakamchaka wa Wakili Muhoja ni wa kipekee kwani akitoa kazi lazima aifuatilie na huo mchakamchaka ndio umesababisha maendeleo hayo. Aliongeza.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mhe. Methew Nganyagwa amempongeza Mkurugenzi Muhoja kwa usimamizi na ubora wa miradi hiyo aidha ameagiza kuandaliwe makala maalumu ili kuonesha ubora wa miradi ya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Lumuli Mhe. Yohanes Mlusi ambaye pia ni mjumbe wa kamati hiyo amempongeza Mkurugenzi Mtendaji na kusema kuwa ilikua ni kama ndoto kuwa na majengo ya kisasa yanayovutia kwa ubora hasa ukizingatia utekelezaji unafanyika kijijini kitu ambacho kwa kawaida ilikua ni kama haiwezekani.

"Mimi binafsi na wananchi wangu tunashangaa sana yani hatujawahi kuona madarasa ya malumalu, majengo ya ubora wa viwango vya juu, kwa kweli hongera sana Mkurugenzi". Amesema Mhe. Mlusi.

Shukrani na pongezi nyingi pia zimekwenda kwa Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mhandisi Nicco Kasililika ambae amekuwa mtendaji na msimamizi mkubwa wa miradi yote inayktekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa.

Akijibu pongezi hizo Mkurugenzi Mtendaji Wakili Muhoja ameshukuru kwa kupewa pongezi hizo na kusema kuwa mafanikio yote haya ni kwa sababu ya ushirikiano anaoupata kutoka kwa Wahe. Madiwani na kuwaomba kuendelea kutoa ushirikiano pale wanapohitajika kwani Halmashauri ni ya watu wote.

Miradi iliyotembelewa na kukaguliwa na Kamati hiyo ni pamoja na Mradi wa madarasa mawili yanayopatikana katika Shule ya Sekondari Muhwana, Kituo cha Afya Magulilwa, Jengo la Makao Makuu ya Halmashauri linalopatikana katika Kijiji cha Ihemi Kata ya Mgama, Ujenzi wa chumba kimoja cha darasa katika Shule ya Sekondari Lyandembela na Ujenzi wa Kituo cha Afya Kibena.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa