• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KAMATI YA MENEJIMENTI YAFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI

Imewekwa : February 5th, 2024

Kamati ya Menejimenti ikiongozwa na Mwl. Peter Fussi Afisa Elimu ya Awali na Msingi, akiwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, imefanya ziara ya kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na Halmashauri, kwa Robo ya Pili kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024.

Baadhi ya miradi iliyotembelewa ni pamoja na Shule ya Msingi Lupembelwasenga iliyopo Kata ya Mgama, ambapo kuna mradi wa ujenzi wa vyoo. Mradi huo umetekelezwa kwa kiasi cha fedha Shilingi Milioni 42 kwa ajii ya ujenzi wa vyoo vya wanafunzi na walimu matundu 34 ikiwa wavulana matundu 16 na wasichana matundu 16, Walimu matundu 2, pamoja na ujenzi wa mnara wa kuhifadhia tanki la maji.

Mradi ulianza mwaka 2021/2022 na kwamba umekamilikwa kwa 100% na sasa vyoo hivyo vinatumika.

Changamoto iliyopo katika shule hiyo ni uhaba wa maji, hivyo Kamati imeshauri washirikishwe wananchi katika ujenzi  matanki ya chini kwa ajili ya kuvuna maji ya mvua.

Kamati imeendelea na ziara hadi katika shamba la Parachichi lilipo katika Kata hiyo ya Mgama Kijiji cha Ibumila.

Akitoa taarifa ya mradi huo Afisa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Bi. Lucy Nyallu amesema, “Kiasi cha Shilingi Milioni 25 kilitengwa kwa ajili ya kulima shamba hilo na kupanda miche ya Parachaichi. Shamba hilo lina ukubwa wa Heka 45, lakini maparachichi yamepandwa kwa Heka 12 tu, ambapo awamu ya kwanza ilipandwa miche 600 na sasa hivi miche hiyo ina miaka mitatu na imeanza kutoa matunda. Awamu ya pili ilipandwa miche 350 ina mwaka mmoja”.

Kamati imeshauri shamba liwekewe uzio kwa ajili ya kuimarisha ulinzi. 

Katika Kata hiyo pia Kamati imetembelea mradi wa mabwawa manne ya samaki. Akitoa taarifa ya mradi huo Bi. Nyallu amesema, “kilitengwa kiasi cha Shilingi 116,351,200 kwa ajili ya kutekeleza mradi huo. Hadi sasa mabwawa manne yamejengwa, jengo la darasa na stoo kwa ajili ya kujifunzia. Mradi ulianza Januari 2023, na unategemewa kukamilika Januari 2024. Hadi sasa mradi umefikia 99%.

Bi. Nyallu amesema, “bwawa moja lina uwezo wa kuchukua vifaranga wanaozaliana 2,400 na wasiozaliana 3,600. Na kwamba hadi kuvuna samaki hawa inachukua miezi 7 – 8. Samaki watakaofugwa hapo ni aina ya pelege ambao wanafafana na sato. Hii ni kutokana na ukubwa wa soko na hali ya hewa”.

Kadhalika Kamati imetembelea mradi wa ujenzi wa vyoo katika Shule ya Sekondari Lumuli iliyopo Kata ya Lumuli. Ujenzi huu ulichangiwa na wananchi kwa kiasi cha Shilingi Milioni 3,200, na Halmashauri imechangia kiasi cha Shilingi Milioni 7,390,461 na kufanya jumla ya Shilingi Milioni 10,590,461. Kiasi kilichotumika hadi sasa katika ujenzi huo ni shilingi Milioni 4,823. Ujenzi ulianza Oktoba 2023, na unategemea kukamilika Januari 2024. Ujenzi umefikia 60%, ujenzi unaendelea.

Isitoshe Kamati imefika hadi Shule ya Sekondari ya Ufundi Ifunda, ambapo kuna mradi wa ujenzi wa bweni.

Mradi huu ulipata fedha kiasi cha Shilingi Milioni 130 na kwamba ujenzi ulianza Oktoba 2023 na unategemea kukamilika Januari 20, 2024, maradi umefikia 70%. Bweni lina uwezo wa kuchukua wanafunzi 80.

Kamati imeshauri fundi aongeze kasi ya ujenzi kwani wanafunzi wanakabiliwa na uhaba wa bweni.

 

Matangazo

  • PONGEZI June 24, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) January 03, 2025
  • TANGAZO LA KAZI January 24, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MANENO MAZITO YA MHE. MHAPA WAKATI WA KUVUNJA BARAZA

    June 19, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UTAWALA NA MIPANGO YAFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO KWA ROBO YA NNE

    June 19, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI KWA ROBO YA NNE 2024/2025 WAFANYIKA

    June 18, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa