• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Katibu Mkuu CCM Taifa Aleta Neema kwa Wananchi

Imewekwa : May 31st, 2023

Katibu Mkuu CCM Taifa Aleta Neema kwa Wananchi

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Taifa Ndugu Daniel Chongolo aliagiza kujengwa kwa mabweni katika shule ya sekondari Tanangozi, Pamoja ukarabati wa barabara zinazozunguka vijiji vya Udumuka – Mfukulembe, Ifunda- Udumuka, Ikwega – Udumuka na Bandabichi – Ifunda Tech, Pamoja na Wenda hadi Hospitali ya Mt. Theresa.

Ndg. Chongolo alisema hayo wakati wa ziara yake ya siku mbili katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, ambayo ilianza Mei 29 hadi 30, 2023, kwenye Majimbo yote mawili ya Kalenga na Isimani, ambapo alitembelea na kukagua miradi mbalimbali ya ujenzi wa madarasa na mabweni shule ya sekondari ya wasichana Ifunda, upandaji wa vifaranga katika bwawa la Kata ya Masaka, pia alikagua ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Lyamgungwe.

Aidha May 30, Ndugu Chongolo alikagua barabara ya Kising’a-Ilambilole- hadi Isimani Tarafani, pamoja na kuzindua mradi wa maji uliopo katika Kijiji cha Chamndindi Kata ya Nyang’oro, sambamba na ukaguzi wa mfereji wa umwagiliaji wa Mkombozi uliopo katika Tarafa ya Pawaga.

Ndugu Chongolo katika ziara yake aliweza kuwatembelea baadhi ya Mabalozi wa Shina kwa lengo la kuongea nao na kutatua changamoto zao, ikiwa ni Mjumbe wa Shina Namba 7 wa Kijiji cha Ilambilole ambaye amekuwa akiishi katika nyumba ya kupanga, hivyo kuamriwa ajengewe nyumba yake. Katika zoezi hilo Ndugu Chongolo aliweza kununua kiwanja na kuanza ujenzi wa nyumba hiyo mara moja.

Sambamba na hayo Katibu Mkuu huyo wa CCM Taifa, aliwataka viongozi wa Chama kuanzia ngazi ya Shina hadi Wilaya kuwahimiza wananchi wajiunge na chama hicho ili Ilani ya maendeleo iweze kutekelezwa ipasavyo, kutokana na chama hicho kushika hatamu.

Naye Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi, Bi. Sophia Mjema, alisema kuwa Sekta ya Afya imezindua mfumo wa M-MAMA ambao utakuwa maalumu kwaajili ya kuwasaidia akinamama kupata rufaa kutoka kwenye Zahanati kwenda Vituo vya Afya au Hospitali ya Wilaya, kwa kupiga simu ili waweze kuletewa gari ya wagonjwa.

Pia, Bi. Mjema amesema kuwa, mfumo huo utasaidia kupunguza vifo vya akimama na watoto wachanga kutokana na kukumbwa na changamoto za mara kwa mara za kiafya hususani kipindi cha ujauzito na uzazi.

Hata hivyo, Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi wa CCM, aliwataka wakazi wa Mkoa wa Iringa, kuacha kuuza mazao ya chakula hovyo ili waweze kukabiliana na baa la njaa, ikiwa ni pamoja na kuzalisha chakula chenye virutubusho kutokana na kuwepo kwa takwimu za juu za udumavu Mkoani humo.

Akizungumza kwa niaba ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa na Wilaya ya Iringa, Ndugu. Daud Yasin Mlowe, aliwashukuru viongozi wa chama hicho kuamua kufanya ziara katika Halmashauri hiyo, ili kujionea utekelezaji wa miradi ya kimaendeleo na kuahidi kusimamia Ilani ya Chama hicho ili nchi iweze kuwa na maendeleo endelevu.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa