• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Kiasi cha Shilingi Bilioni 60.2 Zapitishwa kwa Bajeti ya 2023/2024

Imewekwa : February 22nd, 2023

Kiasi cha Shilingi za Kitanzania Bilioni 60.2 zapitishwa Katika Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2023/2024

Baraza la Maalum la Madiwani lapitisha Kiasi cha Shilingi Bilioni 60.2 kuwa Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024.

Bajeti hiyo ambayo imekuwa na sura tofauti na kipindi kilichopita, waheshimiwa Madiwani wameipitisha bila kupinga kutokana na umbile lake, kwani imebeba mambo mengi ya msingi hasa miradi ya maendeleo.

Pamoja na kusomwa bajeti ya Halmashauri pia Taasisi nyingine ambazo zipo chini ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa yaani Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) na Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) nao walipata nafasi ya kusoma bajeti zao ambazo zitatekelezwa kwa kipindi cha Mwaka wa Fedha 2023/2024.

Kwa upande wa TARURA wameweza kuweka bajeti ya Shilingi Bilioni 40.089 kwa ajili ya kutekeleza miradi yake, na RUWASA imesomwa bajeti ya Shilingi Bilioni 5.7 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali.

Akitoa hotuba yake fupi Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Veronica Kessy amesema, anampongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri kwa kufanya mchakato wa bajeti hii na kukamilika hatimaye kusomwa na kukubalika.

Aidha Mheshimiwa Kessy hakuacha kugusia suala la wanafunzi wa Kidato cha Kwanza kuripoti shuleni na kutoa siku saba kuanzia tarehe ya leo, wanafunzi wote wawe wameripoti Kidato cha Kwanza, na kwamba kama kuna mtoto ambaye amefichwa au kutoroshwa basi mzazi au mlezi achukuliwe hatua.

Aidha Mheshimiwa Kessy amesisitiza kwa kusema kuwa, “Watendaji wote wa Kata/Vijiji mkishirikiana na Waheshimiwa Madiwani fanyeni ukaguzi nyumba kwa nyumba kuona kama kuna mtoto ambaye hajaripoti shule”.

Mheshimiwa Kessy ameongeza kusema kuwa, utoaji wa chakula shuleni ni lazima sana, kwani itamfanya mtoto aweze kusoma kwa morali kwa sababu atakuwa na uhakika wa kupata chakula cha mchana shuleni. Ameongeza kusema kuwa, wazazi/walezi ni lazima wachangie chakula shuleni, kuwepo na kamati maalumu ya mapokezi ya chakula.

Mheshimiwa Kessy ameendelea kusema kuwa, jambo la lishe ni muhimu kulitekeleza kwani ni agizo na ni agenda ya Serikali Kitaifa. Kila kipindi cha Robo lazima fedha ziidhinishwe ili kutekeleza Afua za Lishe. Mhe. Amempongeza Mkurugenzi Mtendaji kwa kutekeleza Afua za Lishe kwa mwaka wa Fedha 2022/2023 kwa kutekeleza mpango huu wa lishe kwa 100%.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Isimani Mheshimiwa William Lukuvi amewapongeza watendaji wa Halmashauri kwa kufanya kazi vizuri wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji Wakili Bashir Muhoja.

Mheshimiwa Lukuvi ameongeza kusema kuwa, tatizo la Halmashauri hiyo ni mapato kwani ina vyanzo vichache. Hivyo ametoa wazo la kuanzisha vyanzo vingine ambavyo vitaweza kuingizia Halmashauri mapato kama kuwekeza na kukodisha mashamba ya mpunga, mashamba ya miti ambayo itatoa fursa hata kwa kizazi cha baadaye.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri Mheshimiwa Stephen Mhapa amelipongeza Baraza la Madiwani kwa kutoa michango yao na kuhitimisha Mkutano wa Baraza vizuri. Pia amemshukuru Mheshimiwa Lukuvi kwa kuungana na Baraza kwani ni mwakilishi mzuri Bungeni kwa kutetea maslahi ya Halmashauri.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa