• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Kombe La MBOMIPA Lalindima Kwenye Jumuiya Ya Uhifadhi

Imewekwa : October 31st, 2022

Kombe La MBOMIPA Larindima Kwenye Jumuiya Ya Uhifadhi

Na. Zaitun Omary,

Iringa DC.

Shirika la Uhifadhi Tembo Kusini mwa Tanzania (Southern Tanzania Elephant – STEP) kwa kushirikiana na Shirika la Uhifadhi Wanyama Walao Nyama (Lion Landscape), wameandaa Bonanza la Mpira wa Miguu kwa Jumuiya za Uhifadhi kuanzia tarehe 30/10/2022 hadi 11/11/2022 katika Kata ya Idodi kwenye vijiji vya Mapogoro na Tungamelenga.

Lengo la Bonanza hilo ni kwa ajili ya kutoa elimu jumuishi kwa jamii juu Uhifadhi wa Wanyama pori na uhifadhi wa mazingira katika vijiji vinavyozunguka mbuga. Mashirika haya ni wadau wa Uhifadhi Mbuga ya Ruaha, hivyo kutoa ushirikiano kwa Serikali kwa ajili ya kutoa elimu hiyo.

Akizungumza katika ufunguzi wa bonanza hilo, Mratibu na Msimamizi wa miradi ya STEP Ndugu Godfrey Nyangalasa amesema, “tumeandaa bonanza hili kwa lengo la kutoa elimu kwa jamii juu uhifadhi wa wanyamapori na utunzaji wa mazingira, na jamii ione umuhimu na itoe ushirikiano wa uhifadhi wa Wanyama pori na mazingira”.

Bwana Nyangalasa ameendelea kusema kuwa, “Tumeshirikiana na Wadau wenzetu wa Uhifadhi wa Wanyama Walao Nyama (Lion Landscape) ili kuleta ufanishi mkubwa katika jambo hili la uhifadhi”.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Idodi Mheshimiwa Julias Mbuta amesema, “tupo hapa kwa nia moja tu ya kutoa elimu kwa jamii juu ya uhifadhi wa wanyama na mazingira. Bonanza hili litaendelea hadi tarehe 11/11/2022 katika vijiji vyote vinavyozunguka Hifadhi – Mbuga, na mwisho wa siku washindi watapata zawadi, hivyo chezeni kwa furaha”.

Naye Afisa Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Bi. Fatuma Juma alikuwa na haya ya kusema, “kutunza mazingira ni fahari kwa manufaa ya kizazi cha sasa na cha baadae. Bonanza litaendelea katika vijiji 22 vya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ambapo ni Mahuniga, Makifu, Kitisi, Mafuluto, Malinzanga, Isele, Magombwe, Kinyika, Kimande, Itunundu, Mbuyuni, Mkombilenga, Mboliboli, Mbugani, Ilolo, Magozi, Ukwega na Luganga. Baada ya mechi kutakuwa na sinema inayofundisha jinsi ya utunzaji na uhifadhi wa mazingira na Wanyama”, amesema Bi Fatuma.

Baada ya ufunguzi huo ulifuatiwa na mchuano mkali wa mechi ya mpira wa miguu kati ya Kijiji cha Tungamalenga na Kijiji cha Mapogoro, na mshindi amepatikana Kijiji cha Mapogoro kwa kufunga goli moja. Baada ya mechi jioni hiyo wananchi waliburudika kwa kuangalia sinema inayofundisha jinsi ya kuhifadhi Wanyama Pori na mazingira.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa