• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani Yafana Iringa

Imewekwa : December 1st, 2022

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani Yafana Iringa

Kila ifikapo Desemba Mosi dunia huadhimisha Siku ya UKIMWI ili kueneza ufahamu wa ugonjwa wa UKIMWI unaosababishwa na uambukizi wa virusi vya UKIMWI. Ni kawaida kuwa na ukumbusho wa siku hii ili kuikumbusha jamii kuhusu ugonjwa huu na pia kuwajali watu ambao wamefariki kutokana na VVU / UKIMWI. 

Kwa Serikali ya Mkoa wa Iringa imeadhimisha maadhimsiho haya katika Halmashauri ya Wilaya yaIringa Kata ya Mseke Kijiji cha Ugwachanya na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Mkoa, Wilaya, Halmashauri, Wadau, Viongozi wa Dini pamoja na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM).

Akimuwakilisha Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Halima Dendego, Katibu Tawala Mkoa Mhandisi Leonard Robert Masanja amesema maadhimisho ya siku hii yanatoa fursa kwa Serikali, Wataalamu katika sekta mbalimbali, Wanasiasa Viongozi wa Dini na Wananchi kuungana pamoja na kuimarisha juhudi za kudhibiti janga la Virusi vya UKIMWI.

Amesema kauli mbiu ya mwaka huu ni Imarisha Usawa hivyo amesisitiza utoaji wa huduma bora za tiba na matunzo bila unyayapaa na ubaguzi kwa wapokeaji wa huduma hizo yaani ndugu zetu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI.

“Kauli mbiu hii pia ikafanye kazi vizuri kwa wale watu wapya wanaotambulika na kuunganishwa na huduma hizo kwa mara ya kwanza katika vituo vyetu ili waweze kuwa wafuasi bora wa huduma”

Nimefarijika sana na muitikio wenu katika maadhimisho haya kwani inaonesha uwajibikaji wenu na ushiriki katika shughuli za kudhibiti maambuzi mapya ya Virusi vya UKIMWI na UKIMWI mkoani kwetu. Ameongeza.

Aidha amesema jambo kubwa kwa sasa ni utekelezaji wa afua mbalimbali ambazo zitatufikisha kwenye kizazi ambacho hakina maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI, hakina unyanyapaa na hakina vifo vinavyotokana na UKIMWI ifikapo mwaka 2030 kama malengo ya dunia yanavyosema.

“Ni ukweli usiopingika kuwa kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine ni muathirika wa janga hili, kama ndivyo kwa nini tusichukue hatua kama jamii kwa kuwajibika ili tuweze kuepusha vizazi vyetu vijavyo na athari hizi”.

Pia amesema Serikali ya Mkoa itahakikisha inaimarisha mahusiano na wadau na kuendelea kujengea uwezo vituo ili kuweza kutoa huduma bora za tiba na matunzo kwa jamii na makundi yaliyo katika mazingira hatarishi ya maambukizi.

Aidha ametoa maagizo kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri kuendelea kutengea bajeti za mipango na shughuli za kuendeleza huduma za VVU na UKIMWI ndani ya vituo vya Halmashauri ili kuwa na huduma endelevu.

Sambamba na hayo pia amewaagiza Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na Wenyeviti wa Halmashauri kuendelea kusimamia kikamilifu shughuli zote za mapambano dhidi ya UKIMWI katika Wilaya na Halmashauri.

Miongoni mwa mafanikio yaliyopatikana ndani ya mkoa katika utoaji wa huduma za VVU na UKIMWI ni kuongezeka kwa idadi ya vituo vinavyotoa huduma za tiba na na matunzo (CTC), kuongezeka kutoka vituo 63 mwaka 2017 hadi kufikia vituo 184 mwaka 2022.

Pia kuimarika kwa upatikanaji wa dawa, vitendanishi na vifaa tiba kwenye huduma za VVU na UKIMWI ambapo kumesaidia kuondoa malalamiko kwa walengwa na hali sasa hivi ni bora zaidi.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa