• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Bashir Muhoja akiwa katika picha ya pamoja na timu ya wawezeshaji wa mafunzo kutoka TASAF Taifa, na washiriki wa mafunzo ya Uibuaji wa Miradi ya Kutoa Ajira za muda, Kunusuru kaya Maskini

Imewekwa : March 11th, 2022

Timu ya Wawezeshaji Mafunzo kutoka TASAF yawanoa kwa Siku sita Wawezeshaji wa Halmashauri (W) Iringa

Na Ofisi ya Habari na Uhusiano

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja amefanya ufunguzi wa Mafunzo kwa wawezeshaji wa Mamlaka za maeneo utekelezaji kuhusu maandalizi, utekelezaji na Usimamizi wa Miradi ya kutoa ajira za muda chini ya mpango wa kunusuru kaya maskini - TASAF awamu ya tatu kipindi cha pili.

Timu ya wawezeshaji wa mafunzo kutoka TASAF, wawezeshaji wa kitaifa ambao ni wataalamu kutoka Halamashauri mbalimbali wamefika kutoa mafunzo hayo kwa lengo la kuwasaidia wawezeshaji kutoka Halmashauri juu ya mbinu na namna ya kuwasaidia wananchi katika kusimamia shughuli za miradi ya kutoa ajira za muda katika ngazi ya Vijiji.

Akifungua Mafunzo hayo ya siku sita, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja amesema mafunzo hayo ni muhimu na kila mmoja aliepata nafasi ya kuteuliwa kushiriki mafunzo hayo anastahili, hivyo wote kuwa makini katika kipindi chote cha mafunzo

"Natambua kuwa wote mko hapa kwa vigezo sahihi, uko hapa kwa sababu unastahili hivyo sitarajii uje ututhibitishie kuwa tulikosea kukuteua ninaomba muwe makini kwa kipindi chote cha mafunzo".

Ameongeza kwa kusema kuwa, mafunzo hayo ni muhimu sana kwani washiriki hao  wakimaliza mafunzo watatakiwa wakawaongoze wananchi kuibua na kusimamia miradi mbalimbali  ya kutoa ajira za muda katika Kata na Vijiji ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa.

Kadhalika amewataka washiriki wote wa mafunzo kuwa makini katika kipindi chote cha mafunzo watakayopatiwa na wawezeshaji waliofika kwa ajili ya kutoa mafunzo hayo na kuuuliza pale wanapokuwa hawajaelewa ili kusaidia kufanyika kwa kazi nzuri na yenye ufanisi kwa hapo baadae.

"Matunda ya mafunzo haya tutayaona katika vituo vyenu vya kazi, sasa kama utashindwa kuelewa vizuri utashindwa kuwajibika vizuri hapo baadae."

Akisoma hotuba kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bw. Ladislaus Mwamanga, Bi. Godliver Mvanda amesema, utekelezaji wa mpango huu unafanyika katika Mamlaka zote za maeneo ya utekelezaji za Tanzania Bara na Zanzibar na unatarajia kuzifikia kaya milioni moja na laki nne na nusu zinazokadiriwa kuwa na watu zaidi ya milioni saba kote nchini, hii ikiwa ni nyongeza ya kaya laki tatu na nusu ikilinganishwa na kipindi cha kwanza.

Ameongeza kwa kusema lengo kuu la mafunzo haya ni kujenga uelewa wa pamoja kwa wawezeshaji wa mamlaka za maeneo utekelezaji kuhusu uandaaji, utekelezaji na usimamizi wa miradi yenye tija inayokidhi viwango vya kisekta na ubora unaokubalika.

“Ni matumaini yangu kuwa mtayapa umuhimu mkubwa mafunzo haya kwa kushiriki kikamilifu kwa siku zote sita zilizopangwa”. Alihitimisha.

Mwenyekiti wa mafunzo hayo Ndugu Lefdedy J. Msamba ambae ni Afisa Umwagiliaji amesisitiza washiriki kushiriki kikamilifu kuuliza maswali endapo hawajaelewa au kuna utata ili kuelewa na mwisho wa siku kazi nzuri ifanyike katika maeneo ya kazi.

Aidha amewataka washiriki na wawezeshaji kuzingatia muda ili mambo yaweze kwenda kama  yalivyopangwa na pia kutaka ushirikiano kati ya washiriki na wawezeshaji.

Akizungumza katika mafunzo hayo Bi Agatha Lugome ambae ni Mratibu wa Mpango TASAF wilaya amesema anatarajia mafunzo haya yatasaidia kuwajengea uwezo washiriki hao na  kuwasaidia wananchi katika usimamizi wa uibuaji wa miradi mbalimbali ya kutoa ajira za muda chini ya mpango wa kunusuru kaya maskini.

Kikao kazi hiki kinafanyika kwa mara ya kwanza katika eneo hili la mamlaka ya utekelezaji katika mzunguko wa pili wa utekelezaji wa miradi kwa mwaka 2022/2023.

Matangazo

  • TANGAZO LA UJENZI WA JENGO LA UTAWALA KATIKA SHULE YA SEKONDARI MLENGE April 30, 2022
  • TANGAZO LA UJENZI WA CHUMBA CHA KOMPYUTA KATIKA SHULE YA SEKONDARI MLENGE April 30, 2022
  • NECTA YATANGAZA MATOKEO YA DARASA LA SABA PSLE 2021 October 30, 2021
  • KILA LA KHERI KATIKA MTIHANI WENU WA KUHITIMU ELIMU YA KIDATO CHA NNE November 15, 2021
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMISAA WA SENSA MAMA ANNA MAKINDA AWATAKA MAAFISA HABARI WA SERIKALI KUTOA ELIMU YA SENSA YA WATU NA MAKAZI

    May 12, 2022
  • MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA MHE. STEPHEN MHAPA AKIWASILISHA TAARIFA ZA UTEKELEZAJI WA KATA YA NZIHI KATIKA MKUTANO WA BARAZA LA WAH. MADIWANI ULIOFANYIKA KATIKA UKUMBI WA SIASA NI KILIMO

    May 10, 2022
  • MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA WAKILI MUHOJA AKIHUTUBIA KATIKA UFUNGUZI WA MAFUNZO YA SIKU TATU KWA WAWEZESHAJI WA TASAF HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA

    May 10, 2022
  • UGAWAJI WA VIFAA VYA USAFI KWA WATOTO WA KIKE WALIOKO SHULENI WANUFAIKA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI TASAF HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA

    May 07, 2022
  • Tazama zote

Video

FAHAMU KUHUSU UGONJWA WA POLIO, DALILI NA NJIA ZA KUJIKINGA
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mtaa wa Gangilonga

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0767778106

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa