• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

"Tuchague Viongozi Wanaofaa Katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa" - Kihwele

Imewekwa : January 29th, 2024

“Tuchague Viongozi Wanaofaa Katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa” – Costantine Kihwele

“Mwaka huu tutakuwa na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa nchi nzima, hivyo tunatakiwa kuchagua viongozi wanaofaa na watakaotuongoza vizuri na kuweza kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi”. Kauli hii imetolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Iringa Komredi Costantine Kihwele, alipokuwa anaongoza kikao cha uwasilishaji wa taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Iringa, ambao ulifanyika Januari 29, 2024 katika Ukumbi wa Siasa ni Kilimo.

Komredi Kihwele ameendelea kusema kuwa, “nitahakikisha kanuni na taratibu zinasimamiwa vizuri na hakuna mjumbe atakayeonewa katika ngazi zote. Hivyo ni jukumu letu kama Chama kuona kila Kata inashinda katika uchaguzi huo”.

Naye Katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya Ndugu Rehema Mohamed amesema, “anawashukuru timu ya Wataalam wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Wakili Bashir Muhoja kwa ushirikiano aliotoa katika kufanya ziara Wilaya nzima, tukizunguka Kata kwa Kata. Kwamba kwenye kila mafanikio hapakosi changamoto, hivyo changamoto zote zilizojitokeza tumezichukua na kuziwasilisha ngazi za juu kwa ajili ya utekelezaji zaidi”.

Bi. Rehema pia amewashukuru Taasisi za TARURA, TANESCO, RUWASA NA IRUWASA kwa kushiriki vizuri katika ziara hiyo na kuweza kujibu na changamoto zilizojitokeza na kuzifanyika kazi kwa wakati.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Veronica Kess, akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani kwa Kipindi cha Miezi sita amesema, “Naishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutulea miradi mingi ambayo ipo hata nje ya Ilani.”

Sasa hivi matokeo ya wanafunzi kwa hatua mbalimbali yametoka na kwamba ufaulu unaridhisha na kwamba wazazi wajitahidi kuhimiza watoto wasome kwa bidii. Matokeo ya wanafunzi imekuwa kama ifuatavyo kwa mwaka 2023 Darasa la Nne Waliondikishwa ni 8,898, Waliofaulu ni 7,149 sawa na 85%, Darasa la Saba waliondikishwa ni 10,471 na waliofaulu ni 9,079 sawa na 88%, Kidato cha Pili waliondikishwa ni 5,413 waliofaulu ni 4,878 sawa na 89% na Kidato cha Nne walioandikishwa ni 4,254 waliofaulu 3,782 sawa na 89% . na Kwamba hadi sasa walioripoti Kidato cha Kwanza ni 5,752. Wanafunzi ziadi ya 3,000 hawajaripoti. Hivyo wazazi wamehimizwa kupeleka watoto shule hata kama na nguo za nyumbani. Watoto walioenda shule binafsi imeagizwa taarifa zao zipelekwe kwake.

Katika Uandikishaji wa Darasa la Awali, waliotegemewa ni 6,643 sawa na 68%, na Waliotegemewa  Darasa la Kwanza ni 8,953 na waliondikishwa ni 7,526 sawa na 84%.

Kwa upande wa Watoto wenye mahitaji maalum, Darasa la Awali 29 ambapo Wavulana 16, na Wasichana 13, na Darasa la Kwanza ni 12 ikiwa Wavulana 6 na Wasichana 6. Hivyo kuleta jumla ya watoto wenye mahitaji maalum 41.

Mheshimiwa Kessy ameendelea kusema kuwa, wazazi waendelee kuchangia chakula cha watoto shuleni pia kuchangia ujenzi wa hostel ili kunusuru watoto wanaotoka mbali na shule.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja akijibu hoja zilizoibuliwa na wajumbe katika Mkutano huo amesema, maboma yote yaliyopo ikiwa ni ya zahanati au shule yametengewa bajeti kwa mwaka wa Fedha 2024/2025. Mabomba hayo ni yale ambayo yamefikia hatua tayari yameshapauliwa, Halmashauri kazi yake ni umaliziaji tu.

 

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa