• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

"Wananchi ni Wajibu Wetu Kumuunga Mkono Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" - Daud Yassin

Imewekwa : January 28th, 2024

“Wananchi ni Wajibu Wetu Kumunga Mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania” – Daud Yassin

Kauli hii imetolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Iringa Komredi Daud Yassin Mlowe alipokuwa katika ziara ya Kamati ya Siasa Mkoa Januari 27, 2024.

“kutokana na Rais wetu kujali wananchi wake kwa kuleta miradi mbalimbali kama shule barabara, zahanati na hospitali, sisi wananchi kazi yetu ni kumuunga mkono Mheshimiwa Rais katika kila jambo analofanya”

Kamati hiyo imeweza kutembelea miradi mbalimbali katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa na kujionea shughuli za miradi inayotekelezwa katika Halmashauri hiyo.

Shule mpya ya Sekondari ya Mbaliboli iliyopo katika Kata ya Mboliboli, Shule mpya ya Sekondari ya Weru iliyopo katika Kata ya Ulanda na Hospitali Teule ya Tosamaganga iliyopo Kata ya Kalenga.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mheshimiwa Halima Omary Dendego amesema, “namshukuru mwananchi aliyetoa eneo lake kwa ajili ya kujenga shule ya Weru. Huu ni uzalendo kwa nchi yake na kupenda maendeleo. Hivyo kwa ajili ya kumuenzi mwananchi huyu naomba jina la shule libadilike badala yakuitwa Weru shule iitwe Sambala, ambapo ndiyo jina la mwananchi aliyejitolea eneo hili”.

Kamati imeridhia kwa kutoa jina hilo na kuahidi matatizo mengine ya shule hiyo ambayo bado yapo, kama bweni hasa kwa watoto wa kike ambao bado wanatoka mbali na eneo hilo.

katika taarifa ya hospitali ya Tosamaganga Mkurugenzi wa Hospitali hiyo Ndugu Benjamin Mfaume pia amewasilisha ombi la kutokatiwa umeme kwani mashine iliyonunuliwa ya mionzi (CT Scan) inatumia umeme mwingi sana. Pia ombi la kujengewa Kituo cha Polisi kwani usalama wa eneo hilo ni mdogo kwa wagonjwa na wauguzaji.

Aidha, Mtaalamu wa mionzi Sr. Aristridia Muhafi aliweza kutoa maelezo jinsi mashine hiyo inavyofanya kazi.

Pia kamati imefurahishwa sana na huduma zitolewazo katika Hospitali ya Tosamaganga, kwani imekuwa msaada mkubwa kwa wananchi wa Iringa na wananchi wanaotoka nje ya Mkoa.

Kwa kuwa ilikuwa ni siku ya upandaji miti Duniani, Viongozi hao walipata nafasi ya kupanda miti katika Shule Sekondari Weru kwa ukumbusho zaidi.

Mwenyekiti aliweza kuwashukuru wananchi, Madiwani na Uongozi wa Halmashari kwa kuweza kushirikiana katika kutekeleza miradi hiyo.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa