• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Watoto Waomba Wazazi/Walezi Kusikilizwa Shida Zao

Imewekwa : June 16th, 2023

Watoto Waomba Wazazi/Walezi Kusikilizwa Shida Zao

Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika hufanyika kila ifikapo Juni 16 Barani Afrika na Tanzania nzima. Kwa upande wa Halmashauri ya Wiaya ya Iringa Maadhimisho hayo yamefanyika Juni 15, 2023 katika Kata ya Nzihi Kijiji cha Kidamali, ili kuweza kusherehekea Kimkoa ifikapo 16 Juni.

Katika Maadhimisho hayo Watoto wameweza kupaza sauti zao na kuwaomba wazazi/walezi kuwasikiliza pale wanapokuwa na shida pia kushirikishwa katika maamuzi ambapo ujumbe wao walitoa kwa njia ya Risala, nyimbo na burudani mbalimbali.

Mwenyekiti wa Halmashauri Mheshimiwa Stephen Mhapa ambaye alikuwa Mgeni Rasmi kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya amesema kuwa, “sherehe ya leo imenifundisha mambo mengi sana hasa kwenye Risala, ambayo imeongea mambo mengi. Japo hotuba hii ni Mkuu wa Wilaya lakini mimi nimesoma kwa niaba yake. Nawapongeza Watoto kwa kuwasilisha hisia zao na kwamba sisi wazazi/walezi tuna wajibu wa kuyafanyika kazi”.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu, Afya na Maji (Huduma za Jamii) Mheshimiwa Felix Waya amesema, “ili malezi ya mtoto yaweze kukamilika anatakiwa kupatiwa chakula kuanzia akiwa na umri wa mwaka sifuri. Baraza la Madiwani limeweka maazimio kuwa, ifikapo Julai, shule zote ziwe zinachangia chakula ili Watoto wapate lishe na afya katika masomo yao.Hii inatokana na hali ya udumavu iliyopo katika jamii yetu”.

Aidha, Mheshimiwa Waya amewashukuru Wadau kwa kujitoa katika elimu na kuhudumia jamii katika maeneo mbalimbali.

Naye Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Bi. Saumu Kweka ambaye amemuwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, amewashukuru Wadau kwa michango yao ya hali na mali katika kuhakikisha jamii inakuwa salama.

Kwa upande wake Mkaguzi wa Dawati la Jinsia na Watot la Polisi Iringa Inspekta Lidia Sospeter amesema, simu ni chanzo cha ugomvi kati ya baba na mama hadi kupelekea familia kutengana na kusababisha Watoto kuhangaika. Pia wazazi wajitahidi kufuatilia vipindi vya Runinga ambavyo Watoto huwa wanaangalia ili kujua kama wanaangalia vipindi vya aina gani.

Ameendelea kusema kuwa, wazazi wawe na tabia ya kuwakagua Watoto hasa wakati wa kuoga ili kugundua madhira wanayopata. Vilevile wazazi/walezi wawafuatilie Watoto wasipende michezo ya kamari ambayo itawaingiza katika vishawishi.

Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yam waka 2023 yamebebwa na Kauli Mbiu isemayo; “Zingatia Usalama wa Mtoto Katika Ulimwengu wa Kidigitali”.

 

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa