• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu;Uwekezaji akiwa katika Maabara ya Uzalishaji wa Maziwa katika Kiwanda cha Asas kilichopo Mkoani Iringa

Imewekwa : June 23rd, 2020

Waziri  Kairuki agiza wawekezeji Halmashauri ya Wilaya ya Iringa wapelekewe Huduma ya Umeme.

Na Ummi Mohamed (Afisa Habari na Uhusiano,Iringa –DC)

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu;Uwekezaji Mh. Angellah Kairuki  ameiagiza Tanesco kupeleka huduma ya Umeme kwa wawekezaji waliopo ili kuwapunguzia gharama za uzalishaji na uendeshaji wa Kampuni zao.

Kauli hiyo aliitoa alipofanya majumuisho ya ziara yake ya kikazi katika Halmashauri ya Wiliya ya Iringa ambapo aliokea Changamoto hiyo kutoka kwa wawekezaji wa Shamba la mifugo la Kampuni ya Asas lililopo Kijiji cha Nyang’oro na Kamupuni ya Masifio iliyopo Kijiji cha Bandabichi.

Aidha changamoto hiyo iliwasilishwa na Wakurugenzi wa Makampuni hayo wakati wakisoma taarifa fupi ya uwekezaji wao kwa Mh Waziri , na kuelezaji jinsi gani wanashindwa kusonga mbele kutokana na changamoto hiyo.

Baada ya kuona Changamoto kubwa inayowakabili wawekezaji hao inafanana ndipo alipoiagiza Tanesco mkoa wa Iringa kuhakikisha huduma hiyo inawafikia kwa haraka kama ambavyo Serikali imekuwa ikiwaahidi wananchi wake.

 “Nagiza Shirika la Umeme Mkoani Iringa kufikisha umeme kwa Wawekezaji wa Kampuni ya Masifio iliyopo Kijiji cha Bandabichi na Shamba la ASAS lililopo katika Kijiji cha Nyang’oro ili kuwawezesha wawekezaji hawa kuongeza ufanisi katika uzalishaji ili kuongeza ajira kwa vijana wetu wa Kitanzania” aliongeza kuwa;

 “Nimesikia tena na hapa katika taarifa fupi muwekezaji anatumia zaidi ya milioni moja kwa wiki kununua mafuta ya jenereta ili aweze kuendeleza shughuli zake za uzalishaji lakini Juni 22 pia nilipokea changamoto hii kutoka Kampuni ya Asas, kwa kuwa Tanesco mpo katika ziara hii naomba mlifanyie kazi kwa haraka na nitarudi ili kuona limefikia wapi suala hili”alisema Waziri Kairuki.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya Bw.Quentin Robb ameishukuru sana Serikali ya awamu ya tano kwa kada zote kwa jinsi inavyowatendea vyema wawekezaji wa ndani na nje kwa usawa.

Naye Mkurugenzi wa kiwanda cha maziwa cha ASAS Fuad Abri  aliipongeza Serikali kwa kufanya ziara zake mara kwa mara na kupita katika kiwanda chake hali inayopelekea kuona jinsi gani Serikali inawajali na kuwathamini wawekezaji wote.

.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa