• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Ziara ya Mhe. Naibu waziri wa Utumishi na Utawala Bora IDC Mh. Ndejembi

Imewekwa : October 27th, 2022

Mh. Ndejembi Aipongeza Iringa DC kwa Kutatua Kero za Watumishi

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mh. Deogratius John Ndejembi, amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri na Maafisa Utumishi kufanyia kazi madeni ya watumishi ndani ya Halmsashauri zao.

Mh.Ndejembi, amesema hayo wakati akiongea na watumishi wa Halmashauri mbili za Wilaya ya Iringa na Manispaa ya Iringa, kuwa Watumishi wa Umma wana haki ya kupandishwa madaraja ikiwa ni pamoja na kupewa stahiki zao za msingi.

“Muweke utaratibu wa kukaa na kusikiliza kero za watumishi wenu, kisha mzibebe changamoto zao na kuzifanyia kazi” alisema Mh. Ndejembi.

Aidha, Mh. Ndejembi, amewataka Viongozi wa Serikali kutoumizana kwenye mazingira ya kazi kwakuwa ufanisi wa kazi wa mtumishi ndio sifa ya Mkurugenzi au Mkuu wa Idara husika, ikiwa ni pamoja na kuwahudumia wananchi kwa moyo.

Sambamba na hayo, Mh. Ndejembi amewataka watumishi wote wa Umma kufanya kazi kwa mpangilio ikiwa ni pamoja na kuweka utaratibu wa kuandika taarifa ya kila kinachofanyika. (Progress Report).

Ameongeza kusema kuwa, kufanya mawasiliano kati ya mtu na mtu ndani ya Idara au Idara na Idara ili kuondoa mkanganyiko katika utendaji kazi.

Naye Mkuu wa Wilaya Mheshimiwa Mohamed Moyo alikuwa na haya ya kusema; “Tunashukuru kwa kutoa pesa kwa ajili ya ujenzi wa Halmashari ya Wilaya ya Iringa ambayo imejengwa katika Kata ya Mgama Kijiji cha Ihemi. Lakini kuna changamoto ya nyumba za watumishi, hivyo watumishi watatumia gharama kubwa sana katika usafiri, hivyo naomba zijengwe nyumba za watumishi ili wafanye kazi kwa ufanisi.”

Mh. Moyo ameongeza kusema kuwa, amejifunza mambo mengi ya Kiutumishi katika kikao hicho, na kwamba amewaomba watumishi kutosubiri Mawaziri waje ndipo watoe malalamiko yao, ili hali kuna Mkurugenzi ambaye ataweza kushughulika na malalamiko hayo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashari ya Wilaya ya Iringa Wakili Bashir Muhoja, ameipongeza Ofisi ya Utumishi Wilaya kwa kushughulikia vema matatizo ya Watumishi hadi kupelekea kupata tuzo kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022, na kwamba kwa sasa malalamiko ya watumishi yamepungua kwa kiasi kikubwa.

Wakili Muhoja ameiomba Serikali kuongeza bajeti kwa ajili ya mahitaji na stahiki za Wakuu wa Idara na aweze kuwalipa kwa wakati, kwani kwa wakati huu anashindwa kuwatimizia mahitaji yao yote kwa wakati mmoja kutokana na ufinyu wa bajeti.

Pia Wakili Muhoja ameomba kuongezewa ikama ya watumishi kwa Kada mbalimbali kwani kila Idara ina upungufu wa watumishi.

Ameongeza kwa kusema kuwa, mikopo inayotoka Serikali Kuu kwa ajili ya Watumishi haitoshelezi, kwani wahitaji ni wengi na kuomba kuongeza kiasi angalau kila muhitaji apate kulingana na maombi.

Wakili Muhoja amemaliza kwa kuomba vitendea kazi hasa kwa upande wa Watendaji wa Kata. Halmashauri imeweza kununua pikipiki 15 tu hivyo uhitaji bado ni mkubwa sana.  

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • "KILA KATA WEKENI MIKAKATI MAALUMU YA KUPUNGUZA HALI DUNI YA LISHE" - MHE. KHERI JAMES

    May 09, 2025
  • KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA PILI YATOLEWA MEI 01, 2025

    May 08, 2025
  • MBOMIPA Wakabidhi Gari kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori

    May 08, 2025
  • IRINGA DC YAKABIDHI MWENGE WA UHURU KILOLO DC

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa