• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe Za Watumishi |
Iringa District Council
Iringa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo umwagiliaji na ushirika
      • Mazingira na Usafishaji
      • Serikali za Mitaa
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA NA Uhusiano
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Mipango,Utawala na Uchumi
      • UKIMWI
      • Afya Elimu na Maji
      • UMazingira, uchumi na Ujenzi
      • Maadili
    • Ratiba Ya Vikao mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Hudumakwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video za Shughuli Mbalimbali za kiofisi na za Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Ziara ya Mheshimiwa Ridhiwan Kikwete Iringa DC

Imewekwa : November 23rd, 2023

“Serikali Inatengeneza Mifumo Ili Kumrahisishia Mtumishi Katika Utendaji Kazi” – Mh. Kikwete

Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – Utumishi Mheshimiwa Ridhiwan Kikwete amefanya ziara Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Nov 23, 2023 na kuweza kuongea na watumishi kwa kusikiliza kero zao.

“Serikali inaendelea kutengeneza mifumo wezeshi ili kumrahisishia mtumishi katika utendaji kazi wake, na kupata taarifa mbalimbali za kiutumishi, kama kukopa fedha benki, taarifa binafsi. Kupitia mifumo mtumishi anaweza kuomba uhamisho mahali popote alipo na kufanya maombi mengine mbalimbali”.

Mheshimiwa Kikwete ameendelea kusema, Ofisi ya Utumishi inawajibu wa kumkumbusha mtumishi juu ya wajibu wake mahala pa kazi na nje ya kazi, kufuata Kanuni za utumishi wa Umma na stahiki zake.

Aidha Mheshimiwa Kikwete amesema, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassana ameendelea kupandisha vyeo watumishi mbalimbali, kuwabadilishia watumishi miundo kwa zaidi ya watumishi 5,000, kutoa ajira mpya na ajira mbadala. Kwa mwaka huu wa fedha Serikali itatoa ajira zaidi 47,374, 000 kwa Watanzania, pia kuendelea kulipa malimbikizo ya mishahara na madeni mbalimbali yasiyo ya mishahara, kufanya uhamisho.

Pia Mheshimiwa Kikwete amemuagiza Mkurugenzi kuandika barua na kuwasilisha madeni yote yanayodaiwa na Watumishi wake.

Mheshimiwa Kikwete ametoa ombi kwa watumishi kuwa, waendelee kufanya kazi ili tija ya kiutumishi ionekane, kudumisha viapo vya maadili ya kazi na kuacha kufanya kazi kimazoea.

Pia ametoa maagizo kwa kusema, Mamlaka ziendelee kusimamia nidhamu, kuweka malengo bayana ya kiutendaji, na wajibu wa kila mtumishi kuwajibika katika eneo lake.

Mheshimiwa Kikwete amemshukuru Rais kwa kumuamini na kumpa kuwa msaidizi katika Wizara hii. Pia amempongeza Mkurugenzi kwa kusimamia miradi na kuongoza vizuri Halmashauri.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mheshimiwa Stephen Mhapa ameishukuru Serikali kwa kuleta miradi mingi katika Halmashauri, na kuomba kuongeza kwa watumishi katika vituo ambavyo kuna uhaba wa watumishi kama zahanati na shule. Pia uhaba wa Watendaji wa Kata na vijiji ambapo inakuwa tatizo katika kusimamia miradi na hasa ikizingatiwa mwaka ujao kutakuwa na chaguzi mbalimbali za Serikali za Mitaa.

Mheshimiwe Mhapa ameongeza kusema juu ya kikokotoo cha wastaafu ni tatizo, kwani wengi wanapoteza maisha kwa mawazo ya kikokotoo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Wakili Bashir Muhoja amemshukuru Mheshimiwa Kikwete kwa kuja kutembelea Halmashauri pia kuongea na watumishi. Na changamoto zote zilizotolewa amezichukua na kwenda kuzifanyia kazi.

Kadhalika Watumishi hao waliweza kutoa kero zao mbalimbali na Mheshimiwa Kikwete amezijibu na kuziwasilisha sehemu husika kwa hatua zaidi.

Matangazo

  • Heri ya sikukuu ya Pasaka April 19, 2025
  • Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura May 01, 2025
  • Kila la Heri Kidato cha Sita 2025 May 05, 2025
  • KUITWA KWENYE USAHILI WA UBORESHAJI WA DAFTARI JIMBO LA KALENGA NA ISMANI December 06, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KAMPUNI YA CC AIRWELL KUWEKEZA UVUNAJI WA MAJI ANGANI NA HEWA UKAA IRINGA DC

    May 29, 2025
  • BURIANI MHE. FELIX WAYA

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI

    May 24, 2025
  • KIJIJI KWA KIJIJI YATUA KATA YA KIWELE, ULANDA NA NZIHI

    May 22, 2025
  • Tazama zote

Video

Makala kuhusu miundombinu ya elimu
video

Viungo vya haraka

  • FOMU YA USAJILI WA VIKUNDI
  • INGIA KWENYE MFUMO WA VIKUNDI VYA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA
  • Salary slip

Viungo vinavyohusiana

  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais-Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais -Utumishi na Utawala Bora
  • Sekretariati ya ajira
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti kuu ya takwimu huria
  • Tovuti Rasmi ya Rais

Idadi ya watembeleaji duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

https://bachelorthesiswritingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kijiji cha Ihemi

    Anuani ya posta: Po.Box108 Iringa

    Simu ya mezani: 026-2702828/2702585

    Simu ya mkononi: 0757 364 994

    Barua pepe: ded@iringadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Haki miliki @ Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Haki zote zimehifadhiwa